HATIMAYE jamaa wamekubali kuwa straika wa Simba, Emmanuel Okwi, ni hatari na anastahili kupewa tuzo yake ya Mfungaji Bora wa Ligi Kuu Bara msimu huu. Okwi anaongoza akiwa na mabao 19 mpaka sasa akifuatiwa kwa mbali na pacha wake, John Bocco ambaye ana mabao 14. Straika wa Mbeya City, Eliud Ambokile, mwenye mabao 9 amesema Okwi ana kasi kubwa ya kuzifumania nyavu hivyo, anaamini ndiye atachukua Kiatu cha Dhahabu. “Bila kupepesa macho nimesalenda na kumpa asilimia kubwa Okwi kubeba tuzo msimu huu, ametuacha mbali sana na ukitazama anavyocheza hawezi kupitwa tena,” alisema. “Malengo yangu ni kumaliza msimu nikiwa na mabao 16, siwezi kuingia kwenye mbio za kuwania Kiatu cha Dhahabu kwa sasa, kiuhalisia ni ngumu na kwa Okwi njia ni wazi kwake.” Nyota mwingine aliyempa kura Okwi ya kuwa mfungaji bora kwa msimu huu ni Khamis Mcha wa Ruvu Shooting, aliyedai straika huyo yupo kwenye moto kweli kweli katika kufumania nyavu. “Kiukweli Okwi msimu huu yupo vizuri, ana asilimia kubwa ya kuchukua kiatu cha ufungaji bora, kiwango chake kipo juu na timu inamwezesha kufikia malengo yake,” alisema.
Jumamosi, 5 Mei 2018
OKWI APEWA KIATU CHA DHAABU KABLA YA LIGI KUISHA
HATIMAYE jamaa wamekubali kuwa straika wa Simba, Emmanuel Okwi, ni hatari na anastahili kupewa tuzo yake ya Mfungaji Bora wa Ligi Kuu Bara msimu huu. Okwi anaongoza akiwa na mabao 19 mpaka sasa akifuatiwa kwa mbali na pacha wake, John Bocco ambaye ana mabao 14. Straika wa Mbeya City, Eliud Ambokile, mwenye mabao 9 amesema Okwi ana kasi kubwa ya kuzifumania nyavu hivyo, anaamini ndiye atachukua Kiatu cha Dhahabu. “Bila kupepesa macho nimesalenda na kumpa asilimia kubwa Okwi kubeba tuzo msimu huu, ametuacha mbali sana na ukitazama anavyocheza hawezi kupitwa tena,” alisema. “Malengo yangu ni kumaliza msimu nikiwa na mabao 16, siwezi kuingia kwenye mbio za kuwania Kiatu cha Dhahabu kwa sasa, kiuhalisia ni ngumu na kwa Okwi njia ni wazi kwake.” Nyota mwingine aliyempa kura Okwi ya kuwa mfungaji bora kwa msimu huu ni Khamis Mcha wa Ruvu Shooting, aliyedai straika huyo yupo kwenye moto kweli kweli katika kufumania nyavu. “Kiukweli Okwi msimu huu yupo vizuri, ana asilimia kubwa ya kuchukua kiatu cha ufungaji bora, kiwango chake kipo juu na timu inamwezesha kufikia malengo yake,” alisema.
Tags
# MICHEZO

About Smartdesmart
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of soratemplates is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.
MICHEZO
Lebo:
MICHEZO
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni