Mwanamuziki aliyewahi kutamba na nyimbo za Uhali Gani, Si Ulinikataa, Nikilala Naota na nyingine nyingi, Q Chillah ameghairi kuachana na muziki kama alivyotangaza awali baada ya kupata mfadhili aliyetangaza kuwa atamsaidia kumrudisha kwenye chati. Chillah amesema alikusudia kuachana na muziki kwa sababu alipotezewa na wadau wa muziki akidai kuwa wapo wengine walikosea, lakini walirudishwa katika mstari akimtolea mfano Saida Karoli na Ruby ambao sasa wanafanya vizuri. Akizungumzia sababu ya kusikitisha uamuzi huo mzito anasema: “Niliona nakuwa mtumwa wa makosa yangu nikaona bora niutue mzigo huu, nikiwatazama watoto wangu nilijiona na madeni, sipo kwenye dunia ambayo wenzangu wapo.” Hata hivyo uamuzi huo ulifikia tamati baada ya kuaminishwa kuwa tasnia bado inamhitaji, hivyo alibadili uamuzi wake. “Tangu nimetangaza kuacha muziki, nimeona mapenzi ya Watanzania, nimeona mahaba yao, mpaka nimejiuliza tatizo sio ‘support’ yao, labda ni mimi au sikupata msaada niliohitaji ili kufanikisha maendeleo ya kazi yangu.”
Jumamosi, 26 Mei 2018
qchila. aghairi kuacha mziki,apata mdhamini
Mwanamuziki aliyewahi kutamba na nyimbo za Uhali Gani, Si Ulinikataa, Nikilala Naota na nyingine nyingi, Q Chillah ameghairi kuachana na muziki kama alivyotangaza awali baada ya kupata mfadhili aliyetangaza kuwa atamsaidia kumrudisha kwenye chati. Chillah amesema alikusudia kuachana na muziki kwa sababu alipotezewa na wadau wa muziki akidai kuwa wapo wengine walikosea, lakini walirudishwa katika mstari akimtolea mfano Saida Karoli na Ruby ambao sasa wanafanya vizuri. Akizungumzia sababu ya kusikitisha uamuzi huo mzito anasema: “Niliona nakuwa mtumwa wa makosa yangu nikaona bora niutue mzigo huu, nikiwatazama watoto wangu nilijiona na madeni, sipo kwenye dunia ambayo wenzangu wapo.” Hata hivyo uamuzi huo ulifikia tamati baada ya kuaminishwa kuwa tasnia bado inamhitaji, hivyo alibadili uamuzi wake. “Tangu nimetangaza kuacha muziki, nimeona mapenzi ya Watanzania, nimeona mahaba yao, mpaka nimejiuliza tatizo sio ‘support’ yao, labda ni mimi au sikupata msaada niliohitaji ili kufanikisha maendeleo ya kazi yangu.”
Tags
# HABARI ZA MASTAA

About Smartdesmart
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of soratemplates is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.
HABARI ZA MASTAA
Lebo:
HABARI ZA MASTAA
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni