MTANZANIA EBORA IMEINGIA,NJIA ZA KUZUIA , KWANINI EBORA INAKUJA MARA KWA MARA - Smartdesmarttz

BELIEVE WHAT YOU HAVE(MWANZO MGUMU)

Jumatatu, 14 Mei 2018

MTANZANIA EBORA IMEINGIA,NJIA ZA KUZUIA , KWANINI EBORA INAKUJA MARA KWA MARA


Virusi vya Ebola vimechomoza tena, mara hii katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Wakati ni vigumu kutabiri ni wapi au lini tena mlipuko huu unaweza kuzuka, ni wazi kuwa tunafahamu mengi sasa kuhusu namna ya kuzuia janga kutokea. Taarifa kuhusu kutokea mlipuko wa Ebola katika mji wa Bikoro kaskazini magharibi mwa Congo mara moja inaleta katika akili jinsi janga hilo linalotisha lililosababisha vifo vya watu 11,000 na wengine 28,000 kuambukizwa katika eneo la Afrika magharibi kati ya mwaka 2014 na 2016. Ni jinamizi ambalo hakuna anayetaka kulishuhudia au kulipitia tena. Watu 600 watoweka kufuatia maporomoko Sierra Leone Maisha baada ya janga la Ebola Afrika Magharibi Tangu Aprili 4 nchini Congo, kumeripotiwa zaidi ya visa 30 ambavyo huenda ni vya ugonjwa wa Ebola - ikiwemo vifo vya watu 18 - licha ya kwamba ni visa viwili tu vilivyothibitishwa kutokana na Ebola. Basi ni kwanini Ebola hurudi mara kwa mara na ni jitihada gani zinazochukuliwa kuzuiwa kurudi upya kwa janga lililoshuhudiwa Afrika magharibi? Hauwezi kudhibitiwa Ebola unaweza kusambaa kwa kasi kupitia kugusa maji maji ya kutoka mwilini mwa muathiriwa. Dalili za kwanza zinazokuja kwa mfano wa homa sio rahisi kuzitambua. Janga la Afrika magharibi mnamo 2014-16 lilizuka katika kijiji kimoja cha mpakani nchini Guinea, na muathiriwa wa kwanza anadhaniwa kuwa mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka miwili aliyefariki duniani mnamo 2013. Haki miliki ya pichaGOOGLE Image caption Mlipuko wa mwisho wa Ebola mnamo 2017 ni mojawapo ya milipuko 9 iliyoshuhudiwa DR Congo Ugonjwa huo ulisambaa nchini Guinea na nchi jirani Sierra Leone na Liberia, na kupindukia ulipofika maeneo ya mijini. Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo ipo maelfu ya maili kutoka mataifa ya Afrika magharibi yalioathirika na janga hilo. Kwamba janga hilo limezuka upya katika eneo la mbali sio jambo la kushangaza. Virusi vya Ebola vimegunduliwa katika miaka ya nyuma mnamo 1976 katika milipuko miwili ambapo watu 151 walifariki katika enoe la Nzara, Sudan kusini na watu 280 waliofariki katika eneo la Yambuku karibu na mto Ebola uliopewa jina kutokana na ugonjwa huo. Haki miliki ya pichaSCIENCE PHOTO LIBRARY Image caption Virusi vya Ebola katika seli iliyoathirika Mlipuko huu wa sasa unafuatia mingine 8 iliyoshuhudiwa DR Congo. Kwa jumla kumeshuhudiwa milipuko 24 - ukiongezwa na wa kati ya 2014 -16 katika Afrika magharibi na kati ikiwemo katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Uganda, Sudan na Gabon. Wakati tunapoyatambua maeneo yalio katika hatari kubwa, itakuwa sio uhalisia kufikiria kuwa ugonjwa wa Ebola utawahi kuangamizwa kabisa na ni vigumu kujua ni wapi au lini mlipuko mwingine unaweza kuzuka. Kutafuta kupuguza maambukizi Tunaweza kuisitisha milipuko kuwa majanga na tunaweza kuboresha mbinu za kuwakinga raia. Hatua ya pamoja na iliyoratibiwa katika kukabiliana na ugonjwa huu inaweza kuhakikisha ugonjwa unadhibitiwa mapema, ili watu wachache iwezekanavyo waugue au wafariki. Haki miliki ya pichaAFP Image caption Maelfu walifariki wakati Ebola uliporipotiwa Afrika magharibi mnamo 2014-16 Ni muhimu kwanza kutambua aina ya virusi na kunakili uwezekano wa maambukizi mapya wakati mlipuko unaporitiwa. Wataalamu kwa mfano kwa mlipuko wa sasa Congo ni lazima watambue chanzo cha maambukizi haraka iwezekanavyo. Watataka kujua mgonjwa huyo amekuwa karibu na nani, na pia ni nani walikuwa karibu na watu hao. Hili ni jambo linalohitaji kufanywa haraka. Muuguzi afariki baada ya wauguzi kuogopa kumgusa Waathiriwa na wanaoshukiwa kuambukizwa watatibiwa katika taasisi za afya katika eneo hilo. Hatua za usafi ni muhimu - ikiwemo kufuniko nyuso, na kuvaa magauni na glavu za mikono kuzuia mwili kugusa maji maji ya aina yoyote kutoka kwa muathiriwa. Chanjo zimekusanywa Kuna aina tano ya virusi vilivyotambuliwa vya Ebola, na kilicho hatari zaidi ni kile cha Zaire. Na ndicho kirusi kilichotambuliwa katika mlipuko wa sasa huko Congo ambapo sasa kuna chanjo ilio tayari kwa matumizi ya dharura. Haki miliki ya pichaCENTERS FOR DISEASE CONTROL AND

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni